Wanafuzi wa darasa la tano wajifunza somo la sayansi kwa vitendo
Wanafunzi wa
Darasa la Tano walifanya somo la Sayansi kwa njia ya vitendo wakijifunza kuhusu
mfumo wa mmeng’enyo wa chakula kupitia uchunguzi wa kuku. Shughuli hii iliwapa
fursa ya kuona kwa uhalisia sehemu mbalimbali za mfumo wa mmeng’enyo na kuelewa
kazi zake katika mwili wa kiumbe hai.
Kupitia somo hilo, wanafunzi waliweza:
Kutambua sehemu
kuu za mfumo wa mmeng’enyo wa chakula
Kuelewa mchakato
wa mmeng’enyo kwa njia ya vitendo
Kukuza ujuzi wa
uchunguzi na kujifunza kwa uzoefu halisi
Shule inaendelea
kutumia mbinu shirikishi na za vitendo ili kuimarisha uelewa wa wanafunzi
katika Sayansi na kuwajengea msingi imara wa maarifa.
Ofisi ya
Taaluma itaendelea
kusimamia utekelezaji wa masomo ya vitendo ili kukuza ubunifu, udadisi, na
ufaulu wa wanafunzi.